Monday, August 5, 2013

JOHN TENDWA SI MSAJILI WA VYAMA TENA NAFASI YAKE YACHUKULIWA NA JAJI MUTUNGI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Jaji Francis S.K. Mutungi kuwa Msajili wa Vyama vya Siasa.

Taarifa iliyotolewa na Ikulu leo Agosti 5, 2013, imesema kuwa uteuzi huo ulianza Ijumaa iliyopita Agosti 2, 2013.

Jaji Mutungi anachukua nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Msajili wa Vyama vya Siasa, Mhe. John Tendwa ambaye amestaafu Utumishi wa Umma kwa mujibu wa sheria.
Source;Jamii Forum

0 comments:

Post a Comment