Siku
moja baada ya Shirikisho la Soka Tanzania kutoa tamko kuwa kama
Yanga itaendelea na msimamo wa kupinga au kukataa udhamini kampuni ya
Azam Media ambayo imepewa dhamana ya kuonesha mechi zote za Ligi Kuu
Bara katika Luninga klabu hiyo haitalamba.....!
mgawo wowote ule wa pesa.
Baada
ya kauli hiyo Uongozi wa Yanga umesema kuwa tatizo la kwawo wao si
pesa bali wao wanachokitaka ni kuwa na uhakika kama Klabu yao
haitahujumiwa au kutotendewa ndivyo sivyo na wadhamini hao katika
Ligi ambao nao pia ni wamiliki wa Timu ya Azam inayoshiriki ligi kuu
Bara.
Mbali
na hilo Kiongozi huyo aliendelea kufafanua kuwa wangependa kuona kuwa
mdhamini wao kampuni ya bia Tanzania (TBL) itatendewa haki kama
walivyokubaliana wakati mabingwa hao waliposaini mkataba.
"Tatizo
letu si pesa, tunataka kuhakikishiwa kwamba hatutachakachuliwa na
kumuweka TBL katika matangazo kabla na baada ya kumaliza mechi zetu,"
alisema kiongozi huyo.
0 comments:
Post a Comment