Friday, August 2, 2013

MBUNGE WA MTWARA MJINI ACHIWA HURU,BAADA YA KUISHIDA SERIKALI MAHAKAMANI.

Mbunge wa Mtwara Mjini (CCM), Hasnain Murji ameachiwa huru dhidi ya kesi ya Uchochezi iliyokuwa ikimkabili,ambayo ilifunguliwa na Serikali...!


Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mtwara jana ilitupilia mbali shitaka la kesi hiyo ya uchochezi wa vurugu za kupinga kujengwa bomba la kusafirisha gesi asilia .

Sababu za Hakimu kufuta mashtaka yaliyokuwa yakimkabili Mbunge huyo ni pamoja hati ya mashtaka iliyowasilishwa mahakamani hapo kuwa na upungufu mkubwa wa kisheria.

Wakili Peter Kibatala,ambae ndie alikuwa akimtetea mbunge wa Mtwara Mjini,alidai miongoni mwa upungufu uliokuwamo kwenye hati hiyo, ni pamoja na kutokuwa na maelezo yanayoonyesha waziwazi kosa alilokuwa akishtakiwa mteja wake.


0 comments:

Post a Comment