Friday, August 2, 2013

WAZIRI AGOMA KUZUNGUMZIA UFISADI WA BILLIONI SABA


Ufisadi wa Shilingi bilioni saba umebainika katika Chama Kikuu cha Wakulima wa Tumbaku Kanda ya Magharibi...!

Imegundulika kuwa, wakulima wamekuwa ‘wakiibiwa’ kwa mfumo wa kupelekewa pembejeo ‘hewa.’ Madai hayo yamebainisha kwamba wanaonufaika na wizi huo kwa wakulima ni vigogo wa Wetcu wakishirikiana na mawakala wanaosafirisha pembejeo hizo.

Mwenyekiti wa muda wa bodi ya Wetcu, Hassan Wakasuvi, alipoulizwa kuhusiana na ufisadi huo alikiri kwamba kuna vyama vya msingi vinadai kwa kuwa vililipa fedha, lakini havikupelekewa pembejeo huku vingine vikikatwa misimu miwili bila kupelekewa pembejeo. “Vingine vilikatwa pesa hata mbolea haikuwafikia, vingine vinadai pembejeo lala yaani walilipa lakini hadi msimu wa kilimo unaisha hawajapata pembejeo.”

Kwa upande wake, Kaimu Meneja Mkuu wa Wetcu, John Kusanja, alisema bodi inahakiki deni hilo ili wawalipe wakulima. Alisema “kuna vyama ambavyo vimelipa zaidi na vingine vililipa pungufu kwa hiyo anayedaiwa atalipa na anayedai atalipwa.”

Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika, Christopher Chiza, alipoulizwa kuhusiana na ufisadi huo alisema yuko kwenye mapumziko na kwamba asingeweza kuzungumza lolote wakati huo.

0 comments:

Post a Comment