Friday, July 26, 2013

KIONGOZI WA CHADEMA KIZIMBANI KWA TUHUMA ZA KUSHIKWA UGONI.


Mwenyekiti wa (Chadema) ambae pia ni diwani wa Wilaya ya.......
Rorya, mkoani Mara katika kata ya Tai, Masirori Kyorang, amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Mwanzo Shirati, akikabiliwa na kesi ya kushikwa ugoni na mke wa mlinzi wa Mbunge wa Jimbo la Rorya.

Masirori alikamatwa Julai 24 kwaka huu katika nyumba ya kulala wageni ya Tripo Kabwana akiwa na mwanamke huyo Pendo Omolo.

Mume wa mwanamke huyo ambaye ni mmoja ya walinzi wa Mbunge wa Jimbo la Rorya katika majengo yake wilayani humo, Ochieng Ninja alipata taarifa ya kuonekana mke wake ndani ya nyumba ya kulala wageni akiwa na Mwenyekiti huyo wa Chadema Wilaya ya Rorya.

mlinzi huyo baada ya kufika katika nyumba hiyo ya wageni aliomba msaada wa watu ambao walijitokeza na kuwakamata mtuhumiwa na mwanamke huyo.

0 comments:

Post a Comment