Monday, July 29, 2013

KIGUGUMIZI CHA VIONGOZI NA MAAFISA HAWA NI WAZI KUWA MADAWA YA KULEVYA NI BIASHARA ZA WAKUBWA WAO.


Ni wazi kabisa  kwamba Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere ,ni kitovu cha kusafirisha dawa za kulevya nje ya nchi,kwani kumekuwa na urahisi na wepesi wa watu hao kupita kwa kuwa tu wanaofanya biashara hiyo ni watu wasiokamatika wala kuzuiliwa ndio maana inaendelea kushamili na kukuwa kila siku.


takribani wiki mbili tu, Watanzania wanne wamekamatwa ughaibuni wakiwa na shehena ya dawa hizo ambazo walisafirisha kutoa Tanzania kwenda nje kupitia uwanja huo bila ya kukamatwa.
Mara ya kwanza walikuwa ni wasichana wawili, Agnes Jerald (25) na Melisa Edward (24), ambao walikamatwa Afrika Kusini na kushtakiwa nchini humo.


Kamanda wa Polisi Kikosi cha Viwanja vya Ndege Nchini, Deusdedit Kato, alisema jalada la upelelezi kuhusu tukio la kukamatwa kwa wasichana Afrika Kusini litapelekwa kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) leo ingawa hakuwa tayari kutaja watuhumiwa ni nani hasa wanaoshirikiana na wafanyabiashara ya dawa

Siwezi kukuambia ni nini kimepatikana katika uchunguzi wala kutaja majina ya watu, kwa kuwa mimi ninapeleka nilichokichunguza kwa sababu naweza kukuambia lakini ikawa sio hivyo kwani huu ni uchunguzi tu,” alisema.

Aliongeza: “Naweza kupeleka jalada langu la uchunguzi kwa DDP lakini kutokana na utalaam wake akagundua kuna mapungufu, hapo tayari nitakuwa nimepotosha umma. Lakini pia akiona upelelezi unajitosheleza yeye ndiye anaweza kuamua kupeleka Mahakamani.”

Nae Waziri wa Uchunguzi, Dk. Harrison Mwakyembe, ambaye amejipatia sifa za utendaji katika siku za hivi karibuni, kwa kuendesha timua timua katika taasisi zinazosimamiwa na wizara yake kwa tuhuma za uzembe, amekuwa kimya na pengine kukwepa kabisa kutia mguu katika sakata la dawa za kulevya JNIA.
Wiki iliyopita Dk. Mwakyembe mwenye dhamana ya Viwanja vya Ndege nchini tulitaka kujua ni hatua gani amechukua, lakini alijibu kwamba hana taarifa za kina kuhusu sakata hilo.


sakata hilo la Madawa ya Kulevya limempa kigugumizi Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Kamishna Robert Manumba, ambaye hakutaka kuzungumzia sakata hilo na kusema liko kwa Kamanda wa Polisi, Kitengo cha Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya, Geofrey Nzowa.

ila sasa Kamanda Nzowa alipoulizwa alisema upelelezi bado unaendaelea kubaini mambo mbalimbali yaliyoko nyuma ya tukio hilo. Alipoulizwa ikiwa Polisi wamebaini mmiliki pamoja na maofisa walioruhusu kupitishwa kwa dawa, Nzowa alisema uchunguzi unaangalia mambo mengi na ndiyo huo utakuja na taarifa kamili.

0 comments:

Post a Comment