Thursday, June 27, 2013

MSANII ALILIA KUIMBA MBELE YA OBAMA


 Ummy Wenceslaus, alimaarufu kama Dokii, ndie anaeililia nafasi ya kuimba mbele ya Rais Barrack Obama pindi kiongozi huyo wa Marekani atakapo tua katika jiji la dare s salaam mwezi ujao.


Dokii anatamani kuimba nyimbo zake mbili za 'No One Like Obama' na 'Obama Welcome to Tanzania' zinazotamba kwenye vituo mbalimbali vya televisheni nchini kwa sasa.

Nyimbo hizo amezitunga maalum kwa kumpongeza na kumkaribisha Tanzania Rais Baraka Obama mwenye asili ya Kenya.

"Nimekuwa nikitunga nyimbo kueleza sifa za Obama tangu anaingia madarakani. Sasa naomba waandaji wa burudani wanipe fursa ya kuimba mbele yake. Nitajisikia vizuri sana," alisema Dokii huku akiweka wazi kwamba bado hajafanya mazungumzo na wahusika wa ziara ya Obama kuhusu ombi lake.
"Kwa sasa niko kwenye mazoezi na 'madansa' wangu tukiamini tutapatiwa nafasi hiyo."

Source Nipashe.

0 comments:

Post a Comment