Monday, June 24, 2013

MAPENZI NI MBEGU ULICHOPANDA LAZIMA UKIVUNE TU,UKITENDA UTATENDWA NA KAMA UTADANGANYA UTADANGANYWA TU



Tunapokuwa kwenye mahusiano ya mapenzi na hata nyakati ambazo mahusiano yetu yanapitia misuguano na tunalazimika kuachana yatupasa tuwe macho sana katika “tunahusianaje” na “tunaachanaje”.

Nina mifano hai ya baadhi ya watu ambao walifikiri mwisho wa ubaya walioutenda wakiwa kwenye mahusiano fulani ungeishia kwenye mahusiano yale tu na wakafikiri mara baada ya kuachana na mpenzi wa zamani na kuanza na mahusiano na mpenzi mpya basi kila kitu kingekuwa shwari kwasababu ya kale yamepita, kwa bahati mbaya yale mabaya waliyoyapanda katika mahusiano yao ya awali yamekuja kuwarudia katika mahusino mengine.

Walitesa, sasa wanateswa, waliumiza, sasa wanaumizwa, walidhulumu, sasa wanadhulumiwa, walidhihaki, sasa wanadhihakiwa, walionea, sasa wanaonewa, na walitenda sasa wanatendwa. Kila unalotenda katika mahusiano yako fahamu kwamba unapanda mbegu, na kama unapanda mbegu basi fikiria pia na wakati wa kuivuna. Always kumbuka kuwa “what goes around comes around”.

Imeandaliwa na Chris Mauki

0 comments:

Post a Comment