Monday, May 13, 2013

UMASIKINI WA AKILI SHAMBA LA WANASIASA,NITATOA MILIONI MOJA KUPIGA VITA UMASIKINI-DR MENGI


Mwenyekiti wa kampuni ya IPP Dr Reginald Mengi amesema kuwa kuanzia mwezi wa tano huu atatoa pesa taslimu kiasi cha shilingi Milioni moja kila mwezi kwa Tweet atakayochagua kuwa bora dhidi ya vita ya umasikini.

Mwenyekiti amesema kuwa lengo lake kufanya hivyo nikutaka kupata mawazo mbalimbali kutoka kwa watu ambayo atayatumia kupiga vita dhidi ya Umasikini unaolitesa taifa la Tanzania na Afrika kiujumla.

Umaskini umekuwa sugu. Kwa mwaka1 anzia Mei ntatoa sh1m kila mwezi kwa tweet nitakayochagua kuwa bora kushinda vita na umaskini”

Umasikini ni jambo ambalo limekuwa kero kubwa sana kwa Mwenyekiti huyo kwani siku ya Jumatano aliandika umasikini wa akili unadumaza uwezo wa kuchambua mambo na kudaikuwa umaskini wa akili ni shamba walitumialo wanasiasa.

Umaskini wa akili unadumaza uwezo wa kuchambua mambo...lipi uongo, lipi kweli. Ndio sababu umaskini wa akili ni shamba la wanasiasa”

0 comments:

Post a Comment