Monday, May 13, 2013

SIRUHUSIWI KUONGELEA CHOCHOTE-LADY JAYDEE



Mwanamuziki Lady Jaydee jana amezuiliwa na Mahakama kuzungumzia jambo lolote lile linalohusiana na Kampuni ya Clouds Media na Viongozi wa kampuni hiyo.

Amri hiyo amepewa jana alipokwenda kusikiliza alichoitiwa Mahakamani hapo baada ya viongozi wa Clouds media kwenda kufungua kesi dhidi yake.

Baada ya kutoka katika Mahakamani alisema hiki

Siruhusiwi kuongelea zile ishu za wale watu niliotofautiana nao mpk mahakama itakapotoa tamko. Hivyo sina jibu la swali lolote kwa sasa.”

Kwamujibu wa Lady Jaydee anapaswa kurudi tena Mahakamani siku ya Jumatatu Tarehe 27 mwezi May siku ambayo tamko litatolewa rasmi na Mahakama juu ya Kesi iliyofunguliwa na viongozi hao wa Redio hiyo.

KUZIBWA MDOMO

Kwa upande wa Lady jaydee alikuwa amepanga kutoa taarifa zaidi juu ya Viongozi hao wa Redio hiyo siku ya Tarehe 16/17 baada ya Kiongozi mmoja wapo kuongea katika Redio yao juu ya bifu yao lakini zikiwa zimesalia siku chache kutolewa kwa taarifa hiyo amri ya Mahakama imemtaka kutozungumza chochote kile juu ya watu hao,kitendo hiki ni sawa na kumziba mdomo mwanadada jaydee.


0 comments:

Post a Comment