Wednesday, May 29, 2013

SINA RAHA KUTOA VIDEO YANGU MPYA WIKI HII-BEN PAUL



Msanii wa RnB kutoka Tanzania Ben Paul ambae ni mzawa wa Dodoma amedai kuwa amekosa raha kusikia msiba wa msaniii mwenzake Albert Mangwea ambae alikuwa akiwakilisha Dodoma katika Game na kama mtu aliewapa Inspiration kufanya muziki hivyo kutokana na msiba huo amearisha kutoa Video yake mpya inayokwenda kwa jina la JIKUBALI ambayo alipanga kuiachia Wiki hii.

Kwa mujibu wa Ben Paul alipanga kuiachia Video hiyo wiki hii na ameamua kupisha Shughuli za mazishi ya Msanii Huyo na zitakapo kwisha ndipo ataachia Kichupa Hicho cha jikubali.

Sidhani kama ninayo raha ya kutoa video yangu mpya wiki hii, naomba radhi, nitapisha shughuli za mazishi ya ndugu yangu “

Alimaliza kwa kusema restInPeace Albert


0 comments:

Post a Comment