Wimbo
mpya wa mwanamuziki Linex unaokwenda kwa jina la Riziki yangu aliempa
shavu Mwanamuziki kutoka Kenya anaewakilisha kundi la Necessary Noise
Wyre ulirekodiwa siku aliyofariki nguli wa muziki wa Taarabu Fatuma
Baraka(Bikidude).
Kwa
mujibu wa Linex amesema kuwa yeye alipata taarifa ya kifo cha
Bikidude akiwa studio anarekodi wimbo huo wa Riziki yangu na alipokea
taarifa hiyo kwa masikitiko.
Siku
kadhaa baada ya kuitambulisha ngoma yake hiyo mpya ya Riziki yangu
imeanza kufanya vizuri katika vituo mbalimbali vya habari.
Na
haya ni maneno machache yanayopatikana katika ngoma hiyo
“Riziki
yangu inapatikana usiku mkubwa wa manane mpaka nitupe ndoano ziwani
ndio nipate chochote,maisha yangu unayajua baby utanivumilia kwenye
shida na raha Ahhhaahh”.
0 comments:
Post a Comment