Friday, February 21, 2014

RAIS WA TFF AKABIDHIWA LESSENI YA OKWI NA CAF

Rais wa shirikisho la soka Tanzania TFF Jamal Malinzi amekabidhiwa lesseni ya Mchezaji wa Yanga Emmanuel Okwi na shirikisho la mpira wa
miguu Afrika.

Jamal Malinzi amesema hayo leo kupitia mtandao wake wa kijamii wa Twitter baada ya kutoka katika kikao cha utambulisho kwa Rais wa CAF Issa Hayatou na katibu mkuu el Amrani, Malinzi aliambatana na Rais mstaafu wa shirikisho hilo Tanzania Leodeger Tenga .

Jamal malinzi ameahidi kuwapa Klabu ya Yanga Lesseni hiyo ya Mchezaji wao Emmanuel Okwi kipindi atakaporudi Tanzania.
CAF wamenipa leseni ya Emmanuel Okwi, nikirudi nchini nitawakabidhi Yanga”


0 comments:

Post a Comment