Thursday, April 4, 2013

RICK ROSS AOMBA MSAMAHA

Mwanamuziki wa Hip Hop kutoka jiji la New York Marekani Rick Ross ameomba msamaha kwa watu wake na wanaharakati mbalimbali kufuatia wimbo wake U.O.E.N.O aliouachia mwezi wa pili mwaka huu kuwa na msitari unaohamasisha vitendo vya ubakaji.
Msamaha aliomba Rick ni baada ya wanaharakati mbali mbali siku ya jumanne kwenda Reebok store iliyopo Manhattan na kutoa mwongozo kwa watengenezaji wa bidhaa za michezo kumtoa Ross kama msanii maarufu wa kuiwakilisha kampuni hiyo katika bidhaa zake.
Katika wimbo huo Ross ame rap kwa kusema “weka kilevi kwenye shampeni yake,hawezi hata kujuwa,namchukua mpaka nyumbani kwake na kufaidi,bila hata yeye kujuwa.
tumewataka Reebok kuvunja biashara na Rick Ross”amesema Shawna Thompson msemaji wa wanawake wa Ultra Violet,kikundi cha haki ya za wanawake kilichofanya maandamano siku ya jumanne akitoa sababu ya kwanini wameamua kufanya hivyo ni kutokana na wimbo huo kuhamasisha vilevi na ubakaji kwa wanamke.
Baada ya sakata hilo Ross Jumanne hii aliomba msamaha kupitia ukurasa wake wa twitter aliposema kuwa “SIFANYI VITENDO VYA UBAKAJI.Naomba msamaha kwa misitari iliyotafisiliwa na kuhusishwa na vitendo vya ubakaji.
SOURCE:CNN

0 comments:

Post a Comment