Waziri
wa uchukuzi na usafilishaji Dr.Harrison Mwakyembe amekiuka sheria kwa
kukiuka masharti ya utoaji zabuni kwa kuipa kampuni inayomilikiwa na
CCM zabuni ya ujenzi wa mradi wa maegesho ya magari makubwa na
makontena.
Inasemekana
kuwa ameipa zabuni kampuni inayoitwa Jitegemee Trading Company
Limited inayomilikiwa na CCM na gharama za Mradi huo utagharimu
Sh.billion 10.
mbali
na kutoa zabuni hiyo Mwakyembe amedaiwa kupeleka mradi huo kujengwa
kwenye eneo la shirika la Uchumi na Kilimo Tanzania SUKITA ambalo
pia linamilikiwa na CCM lililopo Eneo la Tabata.
Mkurugenzi
wa Organaizesheni na Mafunzo wa Chadema, Singo Kigaila, alisema hayo
alipozungumza na waandishi wa habari, jijini Dar es Salaam jana.
Alisema
mradi huo ni kitu kizuri, lakini cha msingi, ambacho kinapaswa
kuhojiwa, unajengwa wapi, na nani na kiasi gani taratibu zimefuatwa.
Kigaila
alisema Halmashauri ya Temeke awali, ilitaka kuingia ubia na Bandari
kujenga mradi huo kwenye eneo la Kurasini, karibu na Bandari, lakini
Mwakyembe ameliacha eneo hilo na kuupeleka kwenye eneo la Sukita.







0 comments:
Post a Comment