Thursday, April 4, 2013

KAMATI ZA BUNGE ZAIBANA MBAVU SERIKALI

ZITTO KABWE
Wabunge wameendelea kuibana Serikali katika vikao vya kamati za bunge vinavyojadili mapendekezo ya Bajeti ya Wizara mbalimbali.
 kumekuwepo na mvutano mkubwa kati ya wabunge juu ya mapendekezo hayo hali inayoashiria kuwepo kwa mvutano mkubwa katika Bunge la Bajeti linalotarajiwa kuanza tarehe 9 mwezi huu wa nne mjini Dodoma.
Misuguano ambayo ilijitokeza jana ni baina ya Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) ambayo ilimgomea Waziri wa Fedha, Dk William Mgimwa kupunguza Bajeti ya Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).
Wakati hayo yakiendelea vile vile Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira ilikataa kupitisha mapendekezo ya Bajeti ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) ya Sh42.7 bilioni kwa maelezo kwamba fedha hizo ni kidogo sana.
Kwa upande wa Mawasiliano Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa aliiwekea ngumu Kamati ya Miundombinu, ambayo ilikuwa ikitaka kuongezwa muda wa matumizi mfumo wa analojia hadi 2015, badala ya mwaka huu.




0 comments:

Post a Comment