Friday, April 5, 2013

MPAKA ULIOPO KATI YA TANZANIA NA MALAWI USIGUSWE


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh Bernad Membe leo akizungumza na waandishi wa Habari ameitaka nchi ya Malawi kuacha kutapatapa na kuheshimu Makubaliano walioyoyafikia kuliachia jopo la usuluhishi la SADC kufanya kazi yake.
Serikali ya Malawi iache kutapatapa. Waheshimu Makubaliano yetu ya kuliachia jopo la usuluhishi la SADC lifanye kazi yake”
Membe aliendelea kueleza kuwa makubaliano kati ya Tanzania na Malawi suala la kwenda au kutokwenda ICJ kutategemeana na hitimisho la Jopo la usuluhishi na sio vinginevyo
Wakati jopo la usuluhishi linaendelea na kazi yake,mpaka itakavyoamuliwa vinginevyo, mpaka ulioko katikati ya Ziwa uheshimiwe na usiguswe

0 comments:

Post a Comment