Tuesday, April 2, 2013

HAKIELIMU WAFUNGUKA JUU YA KUFELI KWA WANAFUNZI


Wadau wa elimu wamesema mengi. Laiti wangesikilizwa, hali ya elimu nchini isingefika hapa ilipo. Kwa bahati mbaya sana, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi haikutoa nafasi kwa mawazo ambayo hayatokani na wao wenyewe, au watu ama taasisi wanazozichagua kuzisikiliza. 

Usipoziba ufa, utajenga ukuta. Hatimaye Tanzania tumeanza kujenga ukuta. Tungeweza kuziba nyufa mapema-kuliko sasa tunapolazimika kujenga ukuta. Sio kutokana na matokeo mabaya tu; ufundishaji na ujifunzaji umeshuka sana katika shule zetu na hali ya elimu nchini inazidi kuwa mbaya; hasa kuanzia elimu ya awali na ya msingi. 

Hebu sasa mdau sema angalau jambo moja muhimu ambalo TUME YA MH. PINDA; au serikali kupitia wizara ya elimu wanapaswa kulizingatia. Wana-HakiElimu tumeanzisha kampeni hii ya kukusanya jumbe fupi fupi za wadau kwa picha; au kwa maandishi; ambazo tutazikusanya na kuzifikisha kwa wadau. 

TUTUMIE PICHA YENYE UJUMBE AU MAANDISHI MAFUPI SASA.



0 comments:

Post a Comment