Sunday, April 14, 2013

BILLIONEA MWINGINE AFARIKI DUNIA ARUSHA

Mfanyabiashara maarufu jijini Arusha Joseph Sambeke mwenye umri wa miaka 49 alimaarufu kwa jina la Bob Sambeke amefariki dunia Juzi kwa ajari ya Ndege ndogo aliyokuwa akiindesha.

Huu ni msiba wa tatu kutokea jijini Arusha kwa wafanya biashara wa jiji Hilo katika mwezi mmoja tu alianza kufariki Wakili na mfanyabiashara maarufu Nyaga Mawalla akafuata mfanya biashara wa madini mkoni humo Henry Nyiti na juzi umauti umemfika Sambeke.

Ndege ya Sambeke aina ya MT 7- namba 5H-QTT ilianguka saa 12.34 jioni baada ya bawa lake kugonga mti katika eneo la Magereza linalopakana na uwanja huo.
Alijeruhiwa na baadaye alifariki akiwa njiani wakati akiwahishwa hospitalini na askari wa Magereza ambao wanaishi katika kambi alipoanguka. Mazishi yake yamepangwa kufanyika Alhamisi eneo la Karanga, Moshi.

0 comments:

Post a Comment