Saturday, March 23, 2013

SITTA APINGA SHUTUMA ZA WABUNGE

SAMWELI SITTA

Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Samweli Sitta amepinga shutuma zilizotolewa na baadhi ya wabunge wa  Jumuiya ya Afrika Mashariki kutoka Tanzania kuwa Wizara yake haina ushukirikiano dhidi ya wabunge hao wawapo kazini.

Wajumbe hao walidai kuwa Sita hana ushirikiano mzuri  kwa wabunge hao wanapokuwa katika shughuli za kikazi, wabunge hao walitoa malamiko hayo Jumanne kabla ya kikao cha kamati ya Mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimataifa  kukaa.
   

Akijibu malalamiko hayo  Naibu Waziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Dr Abdullah J ADDULLAH  alisema malalamiko hayo hayana ukweli wala uhalisia kwani Waziri amekuwa wazi katika utendaji wake,na amekuwa akifanya kazi kubwa ila tatizo lipo kwa wabunge wenyewe.

Baada ya kikao kuisha sitta alikusanya nyaraka zilizoonyesha jinsi alivyokuwa akiwapa taarifa za vikao wabunge hao na walikuwa wakishindwa kuudhuria vikao hivyo kwa kutoa udhuru.

0 comments:

Post a Comment