Friday, March 29, 2013

SHYROSE BANJI ATOA POLE KWA WAFIWA NA MAJERUHI


Mbunge wa Afrika Mashariki Shy-Rose Bhanji ametoa pole leo kufuatia jengo lilianguka kuuwa na kujeruhi watu katika eneo la makutano ya barabara ya Morogoro na Idra ghand jijini Dar es salaam.

Mbunge huyo ameonesha kuguswa na kuumizwa na tukio hilo lililotokea leo majira ya asubuhi na kusababisha vifo kwa watu zaidi ya kumi mpaka sasa na kujeruhi watu zaidi ya thelathini ambao wameokolewa wakiwa Hai na kukimbizwa Hospitali ya Rufaa Mhimbili kwa matibabu zaidi.

“KUANGUKA KWA GHOROFA HAPA DAR: Mungu awape nguvu majeruhi wote, Mungu azilaze mahala pema roho za waliopoteza maisha na tunakuomba Mungu ndugu zetu waendelee kuokolewa wakiwa hai! Pole nyingi kwa wafiwa, jamaa na marafiki. Ni msiba wetu sote”Amesema Shy-Rose.

Kufuatia zoezi la uokoaji linaloendelea katika eneo la tukio kwa mujibu wa ripoti zilizopo mpaka sasa zaidi ya watu kumi wameripotiwa kufariki dunia na wengine zaidi ya thelathini wameokolewa wakiwa wazima ila ni majeruhi waliokimbizwa hospitali

0 comments:

Post a Comment