Saturday, March 30, 2013

SABABU JENGO KUPOROMOKA


Raisi wa Taasisi ya waandisi Tanzania  Malima Bundara amesema kuwa chanzo cha jengo hilo kuanguka jana kuwa imesababishwa na msingi mbovu wa jengo hilo ulioshindwa kuhimili mzigo  wa juu na vifaa vya ujenzi visivyo imara vilivyotumika kujengea

Lakini pamoja na sababu alizozitoa Malima kamanda wa polisi kanda maalumu ya Dar es salaam Sulemani Kova amesema polisi pamoja na bodi ya makandalasi  na bodi ya waandisi watashirikiana kwa ukalibu kuchunguza tukio hilo kwa kina zaidi.

Kuanguka kwa jengo hilo jana si mara ya kwanza katika historia ya tanzania hivi kalibuni kwani mwaka 2008 lilianguka jengo lenye ghorofa kumi maeneo ya kisutu na kujeruhi watu,vilevile mwaka 2006 lilidondoka lingine maeneo ya chang’ombe na kujeruhi watu na bila kusahau juzi juzi hapa kunajengo limedondoka kinondoni na kujeruhi watu na mali zao  

Nikuache ukiendelea kutafakari na kujiuliza kama tatizo ni vifaa vya ujenzi vipo chini ya kiwango maana havina ubhora je mamlaka husika kama TBS ziko wapi na zinafanya kazi ipi?je hivyo vifaa ni kwamba vinaingia kwa njia zipi mpaka vishindwe kuzibitiwa?je  viongozi wetu kweli wanamapenzi ya kweli kwa sisi wananchi wa hali ya chini kabsaa au wanafanya kazi kwa masirahi yao binafsi?




0 comments:

Post a Comment