Saturday, March 30, 2013

ALIE MPIGA RISASI PADRI MUSHI AKAMATWA ZANZIBAR


Polisi zanzibar wametoa taarifa kuwa wamemkamata Omar Mussa Makame mwenye umri wa miaka 35 wakimtuhumu kuwa ndie aliehusika na mauaji ya padri Evaristus Gabriel Mushi alie uwawa kwa kupiga Risasi siku ya Jumapili 17 mwezi wa pili alipokuwa kaielekea kuongoza Misa.

Kamanda wa polisi Zanzibar Mussa Ali Mussa amesema kuwa mtuhumiwa huyo amekatwa jana katika maeneo ya Kariakoo kufuatiwa uchunguzi mkali wa kipolisi uliofanyika na kumpata

Sakata hilo limefuatia baada yua siku mbili toka kardinali Pengo kuwatuhumu polisi kwa uwezo mdogo na kushindwa kabisa kumkamata mtuhumiwa alihusika na mauaji ya padri Mushi.










0 comments:

Post a Comment