Jimbo la Bumbuli Mkoani Tanga
linaloongozwa na Mh January Makamba limepata Halmashauri ya Wilaya
Akizungumza juu ya suala hilo Mbunge
wa Jimbo hilo Mh January Makamba amesema kuwa imemchukuwa miaka miwili
kufanikisha suala hilo
“Hatimaye suala nililolipigania kwa
miaka miwili limefanikiwa kwani Jimbo la Bumbuli sasa limepata Halmashauri ya
Wilaya
Kwa mfumo wa utawala wa nchi yetu,maendeleo
yanapangwa, kusimamiwa na kutekelezwa katika ngazi ya Halmashauri”.
Mbunge huyo aliendelea kuzungumza
kuwa baada ya kujing'atua kutoka katika Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto, sasa
tutakuwa na rasilimali nyingi zaidi za maendeleo, tutakuwa na eneo dogo zaidi
la usimamizi wa shughuli za maendeleo (tulipokuwa ndani ya Halmashauri ya
Lushoto tulikuwa Kata 44.
Sasa tutakuwa Kata 16 tu),
tutasogeza huduma za kiutawala na kijamii karibu zaidi na watu, na tutasukuma
maendeleo kwa kasi zaidi. Kazi iliyo mbele yetu sasa ni kuisimamia vizuri hii
Halmashauri ili malengo yetu yatimie. Kazi hiyo tutaifanya.
Uzinduzi wa Halmashauri hiyo mpaya
itakuwa ni Tarehe 24 Februari 2013.







0 comments:
Post a Comment