Saturday, March 30, 2013

RUSWA INAUWA WASIO NA HATIA


Mchana huu Mbunge wa jimbo la bumburi Mh January Makamba amefunguka na kusema kuwa Rushwa haitajilishi tu yule anaepokea bali inauwa wale wasio na hatia yoyote.

Makamba ameyasema hayo kufuatia kuanguka kwa jengo jana asubuhi na kuwawa Raia wasio na hatia na kujeruhi wengine
“Dua zangu kwa wote ambao wamefukiwa na kifusi baada ya kuporomoka kwa jengo jijini Dar es Salaam jana asubuhi.

Familia za ndugu zetu hawa zinapitia kipindi cha huzuni kubwa sana”
Aliendelea kuzungumza huku akionesha ishara ya kukiukwa kwa mambo mengi katika ujenzi wa jengo hilo  uliokuwa ukiendelea siku ya jana asubuhi kabla ya kuleta maafa ya kuanguka na kuuwa raia

“Kanuni za ujenzi za kiwango cha juu kabisa haziwezi kuizidi nguvu ya ulafi na tamaa ya binadamu! Rushwa haimtajirishi yule tu anayeipokea lakini pia inaua wale wasio na hatia”

Alimaliza kwa kusema hivi “Muuza maziwa anaongeza maji kwenye maziwa, kila mtu anamuongopea mwenzake! Jamii inayoongopa inatengeneza utumishi wa umma ulio sawa na jamii yenyewe”.

0 comments:

Post a Comment