![]() |
| DR HARRISON MWAKYEMBE |
Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe amesema kuwa Serikali
inahitaji injini za kisasa ili kuboresha usafiri wa treni kwa mkoa wa Dar es
Salaam na reli ya kati kwa ujumla ili kupunguza gharama za uendeshaji wa usafiri huo.
Dk. Mwakyembe ameyasema hayo (jana) wakati akiongea na wajumbe wa kamati ya Bunge ya Miundombinu walipotembelea mradi wa reli wa kusafirisha abiria jijini Dar es Salaam .
“iwapo injini hizo zitapatikana Serikali itapunguza gharama kubwa izitumiazo kuendesha usafiri huo kwa sasa kwa kuwa injini zilizopo zinatumia mafuta mengi wakati za kisasa zinatumia mafuta machache na zinakwenda kwa kasi.
Dk. Mwakyembe ameyasema hayo (jana) wakati akiongea na wajumbe wa kamati ya Bunge ya Miundombinu walipotembelea mradi wa reli wa kusafirisha abiria jijini Dar es Salaam .
“iwapo injini hizo zitapatikana Serikali itapunguza gharama kubwa izitumiazo kuendesha usafiri huo kwa sasa kwa kuwa injini zilizopo zinatumia mafuta mengi wakati za kisasa zinatumia mafuta machache na zinakwenda kwa kasi.
Waziri wa
uchukuzi aliendelea kuelezea kuwa
“Gharama za injini hizi ni Dola za Kimarekani milioni 6 ambazo Serikali imeshindwa kuzipata kutokana na uwezo mdogo wa kifedha iliyonayo .Hivyo basi juhudi za pamoja zinahitaji baina yetu sote ili kuiboresha sekta hii ambayo ni mhimili wa ukuaji wa uchumi wa nchi” .
“Gharama za injini hizi ni Dola za Kimarekani milioni 6 ambazo Serikali imeshindwa kuzipata kutokana na uwezo mdogo wa kifedha iliyonayo .Hivyo basi juhudi za pamoja zinahitaji baina yetu sote ili kuiboresha sekta hii ambayo ni mhimili wa ukuaji wa uchumi wa nchi” .
msemaji wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) Midladjy Maez alidai gharama za uendeshaji mradi ni kubwa, hivyo aliomba kuboreshwa kwa njia za treni,pamoja na kumalizia ujenzi
wa vituo vya stesheni za njiani.
“Kwa wakati huu TRL haiwezi
kumudu gharama za uendeshaji wa treni hii, kwa hiyo tunaiomba Serikali itoe
ruzuku ili TRL iweze kupunguza hasara inayoipata kila mwezi.







0 comments:
Post a Comment