Saturday, March 30, 2013

AZAM FC KIBARUANI LEO BILA YA MLINDA MLANGO NAMBA MOJA MWIDNINI ALI


Timu ya Azam FC leo wanajitupa kiwanjani tena kusaka alama ntingine tatu muhimu. Leo Azam FC watakuwepo Mlandizi kupambana na Ruvu Shooting ya Pwani.

 Mechi itapigwa kwenye uwanja wa Mabatini kama kawaida na kikosi cha Azam FC kipo makini kwani Wachezaji wote wako timamu ukiondoa mlinda mlango namba moja Mwadini Ali anaesumbuliwa na mafua

Vilevile wachezaji kama  Abdulhalim Humudi hata kuwepo kikosini leo kwani yupo kwenye  majaribio Jomo Cosmos na David Mwantika ambaye anatumikia kadi nyekundu.

Lakini Faraja kubwa katika kikosi cha leo ni kurejea kikosini kwa Brian Umony ambaye ameyashinda majeruhi yaliyokuwa yanamsumbua.


0 comments:

Post a Comment