Thursday, January 29, 2015

TUNAKUJA KIVINGINE-WEUSI

Na Gerald Kitalima 
Lile kundi la muziki wa Hip Hop Tanzania ambalo mwaka jana limetamba kwa ngoma kibao kali WEUSI limesema kuwa kwa sasa wanakuja na ngoma nyingine ambayo itafungua mwaka kwa kundi hilo ambayo ni ya tofauti kwani katika wimbo huo
wamewashirikisha watu ambao wanatengeneza Couples wasanii hao ni pamoja Jux,Vanessa Mdee,Nahreal,Aikamarealle pamoja na Chinbees.
Joh Makini Mwamba wa kaskazini amethibitisha kufanyika kwa kazi hiyo ambayo inakwenda kwa jina la The Indusrty iliyowashirikisha wakali hao wa Bongo fleva ambao kwa sasa wanatamba na ngoma zao mbalimbali katika media,Joh amekiri wazi kuwa katika kazi hiyo iliyofanyika usiku wa jana kuwa ni kazi nzuri sana na haipaswi kusubiri hivyo itavunja ratiba zao ambazo walikuwa wamejipangia kwa mwaka 2015.


Ahsante baba yetu uliye juu kwa hii zawadi usiku huu,kitu ya hatari nathubutu kusema hii haitasubiri itavunja ratiba zetu ni WEUSI feat Couples The Industry vanessa Mdee,Nahreel Gnakowarawara,Juma_jux ,Aika Marealle,Chinbees".

Nae mkali wa kuvunja chorus kutoka katika kundi hilo la Weusi Gnako amefunguka katika ukurasa wake wa Instragram kuhusiana na ujio wao wa wimbo huo mpya uliofanyika jana usiku na yeye amesisitiza kuwa ngoma hiyo haina haja ya kusubiri inapaswa itoke kwani wameifanya kivingine hivyo watu watarajie ujio mwingine wa Weusi kivingine.

"Hivi sasa ni saa nane na robo usiku,tupo office bado the industry yaaaakhaaa watch them black boy flaaaaa,Nikki wapili,vanessa Mdee,Nahreel,Joh Makini,Juma_jux ,Aika Marealle,Chinbees". haisubiri hiii tunakujaa tena!!!

Weusi ni kundi la muziki wa Hip Hop pia ni kampuni ambayo kwa sasa ni moja la kundi ambalo linafanya vizuri katika tasnia ya muziki wa Hip hop Tanzania.



0 comments:

Post a Comment