Na Gerald Kitalima
Mwanamuziki anayetamba na single yake ya Nakumiss
miss, Timbulo amefunguka na kuweka wazi kuwa katika maisha yake ya
muziki hategemei mahusiano yake ya kimahaba kuwa 'Kiki' ya kazi yake
ya muziki anayofanya.
Timbulo amesema kuwa anaamini katika kufanya kazi
nzuri na kuiacha kazi yake isimame yenyewe ndiyo maana hawezi
kupeleka mambo yake ya mahusiano katika vyombo vya habari.
Timbulo amefunguka hayo katika ile programu yake ya
kuweka wazi historia ya maisha yake kupitia katika mitandao yake ya
jamii.
Timbulo anadai katika maisha yake ya mahaba amepitia
mambo mengi lakini hayupo tayari kuweka wazi mambo hayo na huo ndio
utaratibu aliojiwekea.
Katika simulizi hiyo mkali huyo anadai kuwa katika
kupenda ilifika mahali mpaka baadhi ya watu walimwambia kuwa ana moyo
wa kike ingawa mwanzo hakuweza kuwaelewa watu hao lakini kadri siku
zinavyozidi kwenda anakiri kuwa hivyo.
"Niliwahi kuambiwa nina moyo wa kike, ni kitu
ambacho mwanzo sikukielewa lakini siku hadi siku nimekuwa nakisadiki,
ni vile mimi sio msemaji na siamini kama mahusiano yangu ni kiki ya
kazi yangu ndiyo maana huwa si entertain sana mahusiano yangu kwenye
vyombo vya habari nauacha muziki wangu usimame wenyewe."
Timbulo anadai katika maisha yake ya mahaba anaogopa
sana kipindi cha kuachwa lakini anakili kuwa katika kipindi hicho
ndiyo huwa anakuwa na hisia kali za kuandika nyimbo nzuri na ndiyo
huwa anafanya nyimbo nyingi zaidi akiwa katika hali ya kuachwa kwa
kuwa huwa anakuwa na hisia na katika nyimbo ambazo aliandika katika
hali hiyo zote zimefanya vizuri zilipotoka na kupokelewa vyema na
mashabiki wake.
"Nathubutu kusema najua sana kupenda na huwa
naogopa sana zile scene (part) za kuachana asikwambie mtu ni moja
kati ya nyakati ngumu sana kwenye maisha yangu japo ndiyo wakati
ambao huwa nafanyaga nyimbo nyingi na ofcoz nyingi zimefanya vizur so
naamin ndio wakati ambao huwaga naandika nyimbo nzuri sana maana
huwaga ndo faraja yangu, ......kumpenda mtu huwaga ni dakika kumsahau
sasa ndo kizungumkuti"
Kabla ya kutamba na Nakumiss miss Timbulo alishawahi
kutamba na nyimbo nyingine ikiwemo Domo Langu Zito, Sina Makosa,
waleo wakesho na nyinginezo.
0 comments:
Post a Comment