Tuesday, February 11, 2014

KIPIGO CHA 1-0 CHA MVURUGA KOCHA WA SIMBA

Kipigo cha goli 1-0 kutoka kwa Mgambo JKT kimeonekana kumchanganya kocha wa klabu ya Simba, Zdravko Logarusic, ambaye amekiri kuwa kikosi chake
kina kazi kubwa mbele ya Mbeya City katika mechi ijayo ya Ligi Kuu Tanzania Bara kwenye Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya Jumamosi hii.

Simba juzi ilikutana na kipigo cha 'kustusha' kutoka kwa timu iliyokuwa inaburuza mkia ya Mgambo JKT kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini hapa na hivyo kuteremka kwa nafasi moja kwenye msimamo wa ligi kutoka nafasi ya tatu hadi ya nne ikiwa na pointi 31, tatu nyuma ya Mbeya City iliyo katika nafasi ya tatu.

Loga alisema kuwa baada ya kipigo hicho, timu yake ipo kwenye wakati mgumu kwa sasa wanapoenda kucheza dhidi ya Mbeya City ugenini katika uwanja "mgumu kupata matokeo" wa Sokoine.
Loga alisema kama wangepata ushindi kwenye mechi yao ya juzi ingekuwa chachu ya ushindi kwenye mchezo wao wa Jumamosi dhidi ya City.

0 comments:

Post a Comment