Thursday, December 12, 2013

MKINITOA MADARAKANI NITAFURAHI-MIZENGO PINDA.

Sakata la wabunge kutaka Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi), limechukua sura mpya, baada ya Waziri Mkuu Mizengo
Pinda kuwataka wabunge wamtoe madarakani kama wanaona hafai.

Kauli hiyo imetolewa leo bungeni wakati waziri mkuu alipokuwa katika Kipindi cha maswali na majibu kwa waziri mkuu ndipo alipotoa kauli hiyo na kuongeza kuwa kama itakuwa hivyo yeye atafurahi kwani atakuwa amepata nafasi nzuri ya kupumzika na kuendelea na maisha yake ya kila siku.

Halii hii imefikia kutokana na ukweli kwamba baadhi ya wabunge walikomalia suala la kutaka Waziri mkuu na Waziri wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu wajiudhulu nyazifa zao kutokana na kushindwa kuchukua maamuzi dhidi ya ubadhilifu wa Fedha katika Wizara yao.

Jumamosi iliyopita, wabunge wawili, mmoja wa CCM, Kangi Lugola, (Mwibara) na David Kafulila, (NCCR-Mageuzi Kigoma Kusini), walimlipua bungeni Waziri Mkuu Pinda, wakimweleza kuwa ni mzigo namba moja na wamemtaka Rais Jakaya Kikwete amtimue kazi.


0 comments:

Post a Comment