Mwanamuziki
Fid Q ambaye anawakilisha Mwanza katika Muziki wa HiP Hop na kuibeba
Tanzania katika Hip Hop amefunguka na kuweka wazi kuwa wanasiasa
wa
Tanzania wengi wameweka Masirahi yao mbele kuliko hata maslahi ya
Taifa au watu wanaowatumikia.
Mwanamuziki
huyo ameonesha Kuwapuuza wanasiasa kwakuwa wanachokitenda ni tofauti
na imani yake na kile ambacho yeye anakiamini ila ili kwenda nao sawa
na kutokuvunja heshima yao muda mwingine anajifanya kama hawaoni
wanavyofanya michongo yao ya kupiga pesa za Umma.
“Wanasiasa
wabongo washanidissapoint siku nyiiiiingi sana..Na ili nisionekane
HATER.. Nimeamua kujifanya siwaoni wanavyojipigia 'mahela' yao”
akiwa
anajaribu kufafanua kwa makini suala hili FID Q alisema kuwa Ni
ukweli Hawa wanasiasa wa Tanzania Wana imani yao ile ya ' aaah huyo
mwenyewe angepata hii nafasi angejipa shavu '.
Hivyo kutokana na Imani hiyo ndiyo inayowapelekea Kuifisadi Nchi na kupiga Dili ambazo wanaingiza Pesa kuliko hata kutatua Matatizo ya Wananchi waliowapa Nafasi huku wakitegemea wanasiasa hao kuwa Mabolozi9 wazuri kuwawakilisha na kutatua matatizo yanayowakumbuka katika Jamiii.
0 comments:
Post a Comment