Wednesday, November 27, 2013

PROF JAY ATOA SIRI YA MAFANIKIO YAKE

Msanii Prof Jay alimarufu kama Heavy Weight Mc ambaye anakubalika na kufanya vizuri katika Kazi yake ya Sanaa hususani awapo stejini,amefunguka na
kusema kuwa Mashabiki wake ndio wanamfanya aendelee kuwa Vizuri katika Game na hata katika Maisha ya kawaida.

Asanteni sana MASHABIKI wangu kwa kunisupport na kunifanya kuendelea Kuwa hivi mpaka Leo... Naamini siwezi Kuwa Mimi bila nyinyi... I love u all na nawaahidi sitawaangusha!!!! BLESS.”

Prof Jay kwa sasa hana nyimbo mpya ambayo lakini ni moja kati ya wasanii waliopiga Show Nyingi ambazo kwa Mwaka huu na kuweza kumfungulia Milango mingi ya Mafanikio,japo kuwa mkali huyu hana nyimbo mpya Radioni lakini asimamapo Jukwaani huwapagawisha Mashabiki wake kwa kazi zake zilizofanya Vizuri miaka ya Nyuma na kujikuta akiteka Hisia zas Mashabiki wake hao na kwenda nao pamoja katika Kila mstari na kila Wimbo atakaoimba kwa Steji.

Prof Jay ni moja kati ya Wanamuziki wa Zamani ambaye ameweza kuwa na mafanikio kutokana na kazi yake ya Sanaa mbali na kumiliki Usafiri lakini amefanikiwa kujenga nyumba ya Kisasa Mbezi,na kumiliki Biashara mbalimbali ikiwemo Saloon ambayo ipo Maeneo ya Msasani na kufungua Studio kwa ajiri ya Kurekodi Muziki ambayo mpaka sasa haijaanza kazi Rasmi.

0 comments:

Post a Comment