Wednesday, November 27, 2013

HAMIS KIIZA KUSUGUA BENCHI-BRANDITS


Mshambuliaji Hamis Kiiza wa Yanga yupo katika wakati mgumu wa kusugua Benchi ndani ya Kikosi cha Yanga baada ya Kumzingua Kocha Mkuu wa Yanga
Mholanzi Ernie Brandts kwa kumzushia maneno na kumporomoshea Maneno yenye shombo kocha huyo baada ya Kumalizika kwa Mzunguko wa kwanza wa Ligi.

Kwa mujibu wa Vyombo vya Habari viliwanukuu Didier Kuvumbangwa na Hamis Kiiza kuwa Kocha wao anakinyongo nao hivyo anawapa Muda mdogo wa kuonesha uwezo wao wawapo uwanjani,kutokana na hali hiyo imemlazimu Kocha huyo kutoa tamko kuwa hayupo teyari kumpa Namba Mchezaji asiyefuata maagizo na asiyejituma katika Mazoezi.

"Nilisikia malalamiko yao wakinituhumu kwa mambo ambayo hayana msingi. Mimi ndiye kocha, napanga timu kulingana na uwezo na namna kila mchezaji ndani ya timu anavyoonyesha uwezo wake mazoezini.

Sitaangalia jina la mchezaji, Yanga ina wachezaji wengi, tutatumia walio tayari kufuata maelekezo ya benchi la ufundi," Brandts.

Mbona Kuvumbagu Humzungumzi na wote wamefanya makosa sawa?

Kuhusu swali hili Kocha mkuu wa Yanga Mholanzi Brandits alifunguka na kusema kuwa

"Nimezungumza na Kavumbagu (Didier), ameniomba msamaha kutokana na alichokifanya na nimemkubalia kuendelea na mazoezi ya timu. Kiiza (Hamis) bado sijamwona na sijazungumza naye chochote kwa sasa,"




0 comments:

Post a Comment