Tuesday, November 5, 2013

PICHA 7 MWANAFUNZI ALIYEJINYONGA KUEPUKA AIBU YA KUFELI TENA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE.

Mwanafunzi aliyekuwa akisoma shule ya sekondari  Sabasaba  mjini  Iringa akijiandaa kurudia kufanya  mtihani  wa  taifa  wa kidato  cha nne kupitia  kituo 
cha Krelluu mjini  Iringa Khamis Mkundo  mkazi  wa Mwangata  C katika manispaa ya  Iringa amejiua kwa kujinyonga  kwa kamba kwa kile  alichodai  kuchoshwa na kufeli  mara kwa mara mtihani wa kidato cha nne.


Katika  barua  yake  ndefu aliyoiandika  kijana  huyo amesema  kuwa amefanya  hivyo si kwa kujipendea  ila amechukizwa na hatua yake ya  kufeli mara kwa mara  hivyo  kuamua  kujiua ili  kuepuka aibu katika mtihani ujao ambao anaamini angefeli.





0 comments:

Post a Comment