Friday, November 29, 2013

MWANA FA,AY WAMALIZA TOFAUTI ZAO NA HERMY B

Wakali wa kucheza bila kukunja Goti Mwanafalsafa na AY ambao Mwanzo walikuwa na tofauti kidogo na Produza Hermy B aliyetengeneza ngoma zao kama
Habari ndiyo hiyo,Nangoja ageuke na zingine ambazo zilitengenezwa ndani ya B Hits ,wameweka tofauti zao kando na kuishi tena kama Rafiki kama Zamani.

Kupitia Ukurasa wa Facebook wa Produza Hermy B alionesha kuwa sasa wameamua kumaliza Tofauti zao na kurudia maisha yao ya awali ambapo waliishi kama Marafiki waliokuwa na upendo baada ya kuandika Ujumbe Mfupi uliosomeka


 ‘Friends again’,

huku akiwa ameambatanisha na Link ambayo inaonesha Picha ya Pamoja ya Hermy B,FA na AY
 
Picha hiyo inaonesha Hermy B amemwagiwa Maji inasemekana alimwagiwa ndoo ya maji katika kusherehekea siku yake ya kuzaliwa lakini kuthibitisha hilo Hermy alipost Picha Nyingine ikimuonesha yupo na FA Uwanja wa ndege JNI na kuandika maneno machache yalisomeka hiviiii‘Bday continues’.

Mpitanjia inatoa pongezi kwa rafiki hawa ambao waliweza kushirikiana vizuri mwanzo kikazi zaidi na kufanikiwa kundondosha Ngoma nyingi zilizotingisha africa Mashariki kwa kumaliza tofauti zao.












0 comments:

Post a Comment