Sunday, November 17, 2013

DIAMOND PLATNUM AKUTANA NA PETER WA P SQUARE TAZAMA PICHA HAPA

Licha ya kupigwa vita Msanii Diamond Platnum amezidi kuisafisha Nyota yake ya Muziki kwa kuanza kuliangaikia soko la Kimataifa na kuhakikisha anafanya vyema
kama ambavyo ameweza kufanikiwa kulishika soko la ndani na kusimama katika nafasi za juu kabisaa za wasanii wa ndani ambao wanaongoza kulipwa Pesa nyingi katika Shows.

Diamond Platnum kwa sasa yupo nchini Nigeria akifanya Video ya wimbo wake wa My Number 1 (Remix) ambao amemshirikisa Mkali Davido kutoka Nchini Nigeria.


Akiwa Nchini Nigeria Diamond aliweza kuhudhuria Sherehe za Ndoa ya Kimila ya Peter wa Psquare na kupata nafasi ya kukutana na wakali wengine kibao wa Nigeria akiwemo Emmanuel Adebayo,Iyanya na wengine wengi.

0 comments:

Post a Comment