Wednesday, November 6, 2013

BRANDTS ATANGAZA KIAMA KWA MAAFANDE WA ARUSHA

Kocha Mkuu wa Yanga Ernie Brandts ametangaza kiama dhidi ya JKT Oljoro Maafande wa Arusha pindi watakapokutana kesho katika Mchezo wao
utaokaofanyika uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam.

Brandts amefunguka na kusema kuwa haoni sababu ya kutoshinda mechi ya kesho kwani Hakuna Timu ya kuzuia Yanga kutetea Ubingwa wake kwa mara ya pili mfululizo maneno hayo yamemtoka Kocha wa Yanga baada ya wachezaji ambao walikuwa majeruhi kurejea katika mazoezi na kujipanga kwa ajiri ya Mchezo wa kesho,wachezaji hao ni kama Athumn Idd, David Luhende, na Mbuyu Twite ambao walikosa mazoezi ya awali kujiandaa na mchezo huo wa kesho dhidi ya JKT Oljoro.

Brandts amesema vijana wake wanaendelea kuimarika na kuyashika vizuri mafunzo yake, kwa jinsi timu ilivyo kwa sasa anaamini vijana wake hakuna timu ya kuizua Yanga kutetea Ubingwa wake kwa mara ya pili mfululizo.

0 comments:

Post a Comment