Thursday, October 31, 2013

YANGA KIBARUNI KESHO BILA NIYONZIMA,NIZAR KHALFANI

Kikosi cha Timu ya Yanga kesho kinaingia kibaruani dhidi ya Maafande wa JKT Ruvu kutoka mkoani Pwani ambapo mchezo huo wa Mwendelezo wa Ligi Kuu
Vodacom,Mchezo huo utachezwa katika Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam,lakini kesho Yanga itakosa Huduma kutoka kwa wachezaji wake Haruna Niyonzima na Nizar Khalfan.

Mpaka sasa Young Africans inashika nafasi ya tatu ikiwa na ponti 22 pointi 1 nyuma ya timu zinaongoza mbili za Azam FC na Mbeya City zote zikiwa na pointi 23 zikitofautiana kwa mabao ya kufunga na kufungwa.

Young Africans inahitaji pointi tatu muhimu katika mchezo huo wa kesho dhidi ya JKT Ruvu ili iweze kujikita kileleni na kukalia kiti cha uongozi wa Ligi Kuu kwa kufikisha pointi 25 ambazo zitaweza kufikiwa na timu mbili tu za Azam FC na Mbeya City ambazo zitachezwa mwishoni mwa wiki.

0 comments:

Post a Comment