Thursday, October 31, 2013

DIAMOND PLATNUM AMEKILI KUMZIKA BABAMKWE

Mkali wa My Number One ambaye kwa sasa amefanya Remix ya My Number na Msanii wa Nigeria Davido amefunguka na kuwadhihilishia Watanzania kuwa
alikwenda kwenye Msiba wa Baba Mzazi wa aliyekuwa Mpenzi wake wa zamani Wema Sepetu.
 
Diamond ameamua kufanya maamuzi hayo ya kuweka Picha katika Mtandao wa Instagram kutokana na baadhi ya mashabiki ambao wanamfuatilia kudai kuwa mkali huyo hakwenda kumpa Support Wema kutokana na Matatizo aliyoyapata ya kumpoteza Baba yake Mzazi Mzee Issack Abraham Sepetu ambaye alipatwa na Ugonjwa wa kupooza kabla umauti kukumkuta.

Mwenyezi Mungu alituagiza kuzika na ndio maana leo tuko hapa... na sio kwenda sehemu uliyokuwa unaforce wewe ili kesho upate picha za kuzusha instagram...! Upo...? Nakwambia, wewe ulokuwa unaandika upuuzi kwenye comment...” Diamond akifunguka hapo

kwa mujibu ya Comment ya Diamond ni wazi kuwa huyu mtu aliyezusha kuwa hakutimba msibani alikuwa amempanga mkali huyo kwenda viwanja vingine na kupotezea suala la msiba wa Baba Mkwe wake wa Zamani lakini kwa kuwa amejawa na Busara na kuwa na watu ambao wanamshauri vizuri aliamuwa kumpiga chini na kwenda kushiriki shughuli za Msiba.

0 comments:

Post a Comment