Wednesday, October 30, 2013

VIJANA MILLIONI 2 WANAISHI NA VIRUSI VYA UKIMWI TANZANIA

kwa mujibu wa Takwimu zilizofanywa Nchini Tanzania vijana zaidi ya milioni 2 na laki Sita wenye umri kati ya miaka 15-24 wanaishi na virusi vya Ukimwi.

Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu,Sayansi na Utamaduni (Unesco), Abdoul Coulibaly amesema hayo jana jijini Dar esa Salaam wakati wa uzinduzi wa ripoti ya elimu ya jinsia na afya ya uzazi kwa vijana katika nchi 21 za Mashariki na Kusini mwa Afrika.

Alisema karibu vijana 50 katika nchi hizo huambukizwa virusi vya Ukimwi kila saa moja, huku idadi ya wasichana wakiongoza kwa maambukizi hayo.

Coulibaly alisema idadi hiyo ya maambukizi ya virusi vya Ukimwi kwa vijana kwa Tanzania, inachangiwa  na kutokuwapo kwa elimu ya kutosha ya jinsia  pamoja na VVU na Ukimwi, afya ya uzazi na ukuaji wa binadamu.

Alisema asilimia kubwa ya vijana hawana uelewa wa  masuala ya afya ya uzazi na jinsia, jambo ambalo husababisha kujiingiza  kwenye mapenzi katika umri mdogo na kusababisha kuongezeka kwa mimba za utotoni.

0 comments:

Post a Comment