Kauli ya
shabiki huyo inakuwa mzigo kwa wachezaji wa Yanga kama, Athuman Idd
‘Chuji’, Kelvin Yondani, Mrundi Didier Kavumbagu na
Wanyarwanda
Mbuyu Twite, Haruna Niyonzima ‘Fabregas’ kuhakikisha
wanafanya vizuri na kuokoa maisha ya kijana huyo mwenye miaka 31.
SHABIKI
maarufu wa Yanga, Steven Mwamwala amedai kuwa, kama wakifungwa na
Simba mechi ya Jumapili ijayo itakayochezwa Uwanja wa
Taifa,atajinyonga.
Na akamsisitizia mcheza filamu, Wema Sepetu afike uwanjani kuona mechi ya Simba na Yanga Jumapili ili ampe zawadi yake ya jezi ya Yanga aliyoi gharamiaSh45,000.
Mwamwala ana historia na Yanga ilipopigwa mabao 5-0 aliangua kilio cha nguvu na video zake kusambaa kwenye mitandao ya kijamii.
Kauli ya shabiki huyo inakuwa mzigo kwa wachezaji wa Yanga kama, Athuman Idd ‘Chuji’, Kelvin Yondani, Mrundi Didier Kavumbagu na Wanyarwanda Mbuyu Twite, Haruna Niyonzima ‘Fabregas’ kuhakikisha wanafanya vizuri na kuokoa maisha ya kijana huyo mwenye miaka 31.
Aliliambia Mwanaspoti kuwa: “Nimeandaa kamba ya katani kabisa, nimeificha na siwezi kusema nilipoiweka kama Yanga itafungwa mchezo huo, nitajinyonga ili kupoteza uhai wangu. Unajua inauma sana mnapofungwa, nataka timu yangu ishinde Jumapili ili niwe na amani kwa ushindi wowote ule ilimradi tutoke na pointi tatu.”
Kuhusu, Wema shabiki huyo alisema anampenda sana kama dada yake na anatamani akutane naye.
“Nimemtafuta sana na naomba siku hiyo aje kwa sababu nimemwandalia zawadi. “Nimemnunulia jezi ya Yanga na tayari nimeiandika jina la Wema, imenigharimu Sh 45,000,” alifafanua Mwamwala ambaye anaishi Tabata Segerea jijini Dar es Salaam.Source:Mwanaspoti
0 comments:
Post a Comment