Tuesday, October 15, 2013

MSANII KALA JEREMIAH AMEPATA SHAVU NI BAROZI WA PEPSI COLA TANZANIA

Msanii wa Hip Hop Tanzania Kala Jeremiah ambaye kwa sasa anatamba na ngoma yake Jaribu kujiuliza ambayo,amepata shavu la kuwa Balozi wa Pespsi Cola Tanzania.


Kala Jeremiah amefunguka kuwa amesaini Mkataba na kampuni ya Pepsi hivyo atafanya kazi kama Balozi wa Kinywaji hicho Tanzania.

Nimesainiwa rasmi kuwa balozi wa Pepsi Tanzania, kwa hiyo kuanzia sasa hivi nafanya kazi zote za kibalozi ambazo balozi anatakiwa kuzifanya katika kampuni.”

Balozi huyo mpya wa Pepsi ametaja vigezo vilivyotumika kumpa yeye shavu hilo, “Kwanza wanaangalia tabia ya mtu,yaani kwamba hujawi kupigana na wala hujawahi kuwa na maskendo,lakini pia wanaangalia umati wa watu ulionao na watu wako wanakusikiliza kiaasi gani.”

Amewashukuru fans wake ambao ndio wamempa nafasi hiyo, kwa kuwa kigezo kimojawapo ni kuwa na umati unaokusikiliza, “Mimi nisema nawashukuru mashabiki wangu zaidi kwa sababu wao ndio wamenifanya leo niwe balozi wa Pepsi, kwa hiyo shukurani zangu za dhati ziende kwa mashabiki wangu ambao wamekuwepo kwa ajili yangu siku zote na wamenionesha mapenzi mpaka makampuni mengine wameona kwamba nina watu wengi ambao wananielewa, kwa hiyo ni hivyo.”

Kwa Tanzania sasa Biashara ya Muziki imeanza kukuwa siku hadi siku kwani hata makampuni ya Nyumbani yameanza kuwekeza katika Tasnia za Michezo,Burudani na kubadili mwelekeo wa Maisha ya wanamichezo na wasanii wa nyumbani.

0 comments:

Post a Comment