Mshambuliaji nyota wa
Simba, Mrundi Amisi Tambwe amejigamba kuitandika Timu ya Yanga siku
ya Jumapili ya Tarehe 20 mwezi huu watakapokutana na watani wa
jadi
katika mechi ya Ligi kuu zinazoendelea kuchezwa.
Mbali na kuonesha
majigambo hayo lakini Mshambuliaji huyo amedai kuwa mechi hiyo
itakuwa ni moja wapo ya sehemu ya kutengeneza kumbukumbu na kutimiza
Malengo yake ya kufunga mabao 20 katika Msimu wa Ligi kuu bara msimu
huu.
"Sijabahatika
kuwaona Yanga wakicheza, lakini nafahamu ni timu kubwa na wapinzani
wakubwa wa Simba, ila hilo sijali. Siku tutakayokutana, nitakuwa na
kazi moja tu ya kuwafunga kama ninavyozifunga timu nyingine,"
Alisema awapo dimbani hujipanga nafasi nzuri ili kufunga
mabao, kitu ambacho kimemsaidia kutwaa tuzo kadhaa za ufungaji bora
katika ligi yao ya nyumbani na ile ya Kombe la Kagame, jambo ambalo
anataka kuona likitokea pia katika Ligi Kuu ya Bara.







0 comments:
Post a Comment