Wanafunzi
wawili wa kidato cha nne katika shule ya sekondari Montfort wilayani
Mbarali, wanadaiwa kubakwa na mwalimu wao ambaye alikuwa anafundisha
shule hiyo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Diwani Athuman
alisema tukio hilo lilitokea wiki iliyopita kwa nyakati tofauti
majira ya usiku. Alisema mtuhumiwa huyo aliyekuwa akifundisha katika
shule hiyo masomo ya mawili inadaiwa alitenda kosa hilo kabla ya
kuhamia shule moja ya sekondari wilayani Musoma, mkoani Mara.“Tukio hilo lilitokea baada ya mwalimu huyo kumuita mwanafunzi mwenye umri wa miaka 17 aliyekuwa akijisomea majira saa 9:30 usiku na kisha kumfanyia unyama huo na mara baada ya kitendo hicho alimwita mwanafunzi mwingine aliyekuwa bwenini majira ya saa 4:00 usiku na kisha kumbaka naye pia” alisema.
Alisema mwalimu huyo anashikiliwa na polisi na taratibu za kumfikisha katika vyombo vya sheria ili kujibu tuhuma hizo zinaendelea.






0 comments:
Post a Comment