Kauli
ya Dk Msonde imekuja siku moja baada ya kuripotiwa kuwa, takriban
watahiniwa 3,000 wa kujitegemea wapo hatarini kukosa mtihani huo
kutokana na kutokulipa karo ya mtihani.
Dk
Msonde jana alilieleza kuwa kawaida Necta baada ya kufunga usajili wa
watahiniwa wa kidato cha nne, huangalia kwenye mifumo yao ili
kutambua aliyekamilisha taratibu zote za usajili.
“Sisi
mifumo yetu haina tatizo lolote na watahiniwa wa kujitegemea
hujisajili online (kwa njia ya mtandao), wapo baadhi ya watu huingia
kwenye mtandao wakitaka kujisajili, wakifika kwenye eneo linalotaka
walipe ada wanaacha,” alisema.
Alisema
watu hao kwenye mfumo wa Necta huonekana kuwa wamejisajili, lakini
hawajalipa karo ya mtihani hivyo huwasiliana nao kwa kuwaandikia
barua au ujumbe mfupi wa simu ya mkononi.
“Hizo
barua ziliandikwa mapema sana baada ya kufunga usajili, kwa sasa
hakuna mtu yeyote mwenye tatizo, wote wameshashughulikiwa. Ili
kutatuliwa tatizo lako haikuhitaji hata kuja baraza, wewe ukipiga tu
simu wataalamu wetu wanakushughulikia, sisi hapa tunafanya kazi saa
24,” alisema Dk Msonde:
source:Mwananchi Newspaper







0 comments:
Post a Comment