Friday, September 6, 2013

DAKTARI FEKI ADAKWA KCMC AKITAKA KUMFANYIA UPASUAJI MGONJWA JANA.

Mtu mmoja aliyefahamika kwa Jina la Alex Sumni Massawe (33), alikamatwa jana Majira ya Saa tano za Asubuhi katika Hospital ya Rufaa ya KCMC iliyopo Moshi akiwa katika Maandalizi ya Kumfanyia Upasuaji Mgonjwa..!
ambae amefahamika kwa Jina la Makasi Tipesa ambaye anasumbuliwa na ugonjwa wa Ngozi.

Habari zinasema kuwa kabla ya kukamatwa kwa Alex, mama mzazi wa kijana huyo, mkazi wa Manispaa ya Moshi, Pamvelina Shirima, alikutana na mtuhumiwa huyo katika baa moja maarufu mjini hapa iliyopo eneo la Dar Street na kumtaka ampe kiasi cha Sh. 200,000. cha fedha kwa madai zitatumika kuharakisha mwanaye wa kiume kufanyiwa vipimo vya upasuaji.


Ofisa Uhusiano wa KCMC, Gabriel Chisseo, alisema kuwa daktari huyo aliwekewa mtego na uongozi wa hospitali hiyobaada ya baadhi ya wagonjwa kuripoti kutapeliwa na mtu ambaye amekuwa akijitangaza kwamba ni daktari wa

“Huyu Alex Massawe tulimkamata leo (jana) asubuhi akiwa katika wodi ya upasuaji baada ya kupokea kiasi cha Shilingi 200,000 kutoka kwa Pamvelina Shirima ambaye alimleta mwanaye afanyiwe upasuaji wa ngozi.

WITO WETU Tunawataka wagonjwa wote kufuata taratibu ikiwamo kutokubali kurubuniwa na watu ambao hawajavaa sare wala kuwa na vitambulisho rasmi vya hospitali,” alisema Chisseo.



0 comments:

Post a Comment