Thursday, August 1, 2013

HUU NDIO USHAIDI ALIOTOA MTOTO WA MIAKA MINNE ALIERUBUNIWA KWA KUPEWA SH.100 NA KUBAKWA.

Ndelagakula Romedafee (23)



Tulipofika dukani mshtakiwa alinipa Sh. 100 nikajua kwa sababu tulikuwa tunakaa naye nyumba moja sikuwa na wasi wasi naye, tulipokuwa tunarudi nyumbani alinipeleka kwenye korongo, alinishika kwa nguvu na kunivua nguo zote kisha kunibaka,”alidai na kuongeza kuwa:

Ndipo nikapiga kelele naumia naumia huku nikiwa nimechafuka kwa vumbi wakati mshtakiwa alivyokuwa ananigalagaza huku akinibaka."

kutokana na unyama huo Mahakama ya Wilaya ya Kigoma imemhukumu Ndelagakula Romedafee (23) kutumikia kifungo cha maisha jela kwa kumbaka mtoto wa kike wa miaka minne baada ya kumrubuni kwa kumpatia Sh. 100.

Hukumu hiyo ilitolewa na Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo, David Ngunyale baada ya ushahidi uliotolewa na upande wa mashtaka kumtia hatiani.

"Kutokana na mshtakiwa kufanya unyama huu wa kubaka mtoto mdogo hivi, mshtakiwa unatakiwa kuondolewa katika jamii na kupelekwa gerezani ili ukajifunze kuwa raia mwema katika maisha yako," alisema Hakimu huyo wakati akitupilia mbali utetezi uliotolewa na mshtakiwam huyo ili mahakama isimpe adhabu kali.

Source:Nipashe


0 comments:

Post a Comment