Thursday, July 25, 2013

HIVYI NDIVYO MBUNGE WA UBUNGO JOHN MNYIKA ALIVYOMFANYIA ANDREW CHENGE.


Mbunge wa Ubungo kwa tiketi ya Chadema Mh John Mnyika leo ameamua kuweka hadharani namba ya simu ya Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti Andrew Chenge baada ya Mwenyekiti huyo kusema kuwa Kodi ya kasi za Simu ni sahihi kutokana na utafiti wao.
Leo tarehe 25 Julai 2013 chombo kimoja cha habari kimemnukuu Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti Andrew Chenge (Mb) akisema kwamba uamuzi kuhusu kodi/tozo ya kadi/laini za simu haukuwa wa kubahatisha. Chenge amesema kwamba kamati yake ilifanya utafiti wa kina na kisha kufikia uamuzi wa kuona tozo hiyo ni sahihi.”

Ni muhimu akatakiwa kupitia namba yake 0754782577 atoe maelezo zaidi kuhusu usahihi wa tozo hiyo na aeleze ni wapi wananchi na wadau mbalimbali wanaweza kupata vielelezo vya utafiti walioufanya.
Hii ni mara ya pili kwa Mbunge wa Ubungo Mh John Mnyika kuweka namba za simu za wanasiasa na viongozi wa Serikali ili kuweza kutolea maelezo juu ya kauli zao kutokana na kodi ya kadi ya Simu iliyoamuliwa kulipwa na Wananchi kama njia moja wapo ya kuongeza kipato katika bajeti ya Serikali ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania.
...


0 comments:

Post a Comment