Tuesday, July 2, 2013

HATUTAMBUI SAFARI YA NSA JOB KWENDA CHINA-COASTAL UNION



Sakata la Mshambuliaji Nsa Job wa Coastal Union kwenda Nchini China kwa majaribio ya kusakata kabumbu nchini humo limechukua sura mpya baaada ya uongozi wa Coastal Union kusema kuwa hautambui suala la safari hiyo wala haujui juu mchezaji huyo kwenda China kwa majaribio kwa kuwa hawana taarifa yoyote kutoka kwa mchezaji huyo.


Binslum amesema hawezi kuzungumzia suala la mshambuliaji wa Coastal Union Nsa Job juu ya safari yake ya china haoni kama ni habari kwani timu haina taarifa zozote juu ya safari hiyo.

“Unajua kuna watu wanapenda tu kuonekana na kusomwa kwenye vyombo vya habari, Nsa Job hajatoa taarifa zozote juu ya kuitwa China kwa majaribio inamaana kitu kama hicho hakipo ingawa alinipigia simu kuniambia yupo China cha kuchekesha ameniambia vitu tofauti sitovizungumza hapa.” 

mbali na kueleza suala la mshambuliaji Nsa Job uongozi wa Coastal Union umesema mpaka jumapili wachezaji wa timu hiyo kwa msimu mwingine watakuwa wamefahamika na wale ambao hawatapata nafasi wameshawapa taarifa kwa kuwaandikia barua.
Coastal union inaanza mazoezi kwa ajili ya kujipanga na msimu ujao wa ligi na kuanzia Tarehe 7 mwezi huu watapiga kambi katika Hotel ya Raskazone.


0 comments:

Post a Comment